KIKAO CHA KAMATI MAALUM YA NEC -ZANZIBAR 20/09/2022.

 







NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.


MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,leo ameongoza kikao Maalum cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar.

Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Afisi Kuu ya CCM,Kisiwandui Zanzibar.

Pamoja na mambo mengine Kikao kitapokea na kujadili Mapendekezo ya Wana CCM wanaoomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Wenyeviti wa CCM Wilaya kwa Mikoa ya Zanzibar.

Aidha Kikao hicho Maalum, kimepokea na kujadili kwa kina Taarifa ya kazi za Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya kwa kipindi cha miaka mitano 2017/2022.

Pamoja na hayo Viongozi mbali mbali walioudhuria kikao hicho ni pamoja Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi,Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.

Wengine ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Zubeil Ali Maulid pamoja na Wajumbe wengine wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar.


               


SHAKA- MIAKA 45 YA CCM YAVUNJA REKODI, ASEMA SAMIA NI ALAMA YA USHINDI.


NA IS-HAKA OMAR, MARA.




    KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa , Itikadi na Uenezi Ndg. Shaka Hamdu Shaka akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Sherehe za Maadhimisho ya Kilele cha kuzaliwa kwa CCM yatakayofanyika kesho Mkoani Mara.
(Picha na Is-kaka Omar- Afisi Kuu ya CCM Zanzibar).



NA IS-HAKA OMAR, MARA.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema ndani ya miaka 45 kimesimamia kikamilifu utekelezaji wa Ilani yake iliyoleta maendeleo yenye tija kwa wananchi wa makundi yote.

Hayo ameyaeleza leo Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM Taifa Shaka Hamdu Shaka wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya sherehe za  maadhimisho ya kilele cha kuzaliwa kwa CCM yatakayofanyika Mkoani Mara.

Amesema Chama Cha Mapinduzi kimekuwa ni taasisi imara ya kisiasa barani Afrika kinachowapelekea wananchi wa Mijini na Vijijini maendeleo endeleovu bila kujali tofauti za kisiasa.

Ameeleza kuwa mnamo Novemba 5,1976 Mkutano Mkuu wa pamoja wa Halmashauri Kuu za Taifa za vyama vya TANU na ASP ulifanyika mjini Zanzibar ,uliamua kuvunja vyama hivyo ili kuunda chama kipya ,Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Amesema vyama hivyo vya ukombozi vilivunjwa kwa heshima na taadhima kubwa ,si kwa sababu vilishindwa kutimiza malengo yao,bali ni kwa nia ya kupata chama kimoja kipya,kilicho imara na madhubuti kukabiliana na changamoto za kudumisha umoja wa kitaifa na kulera maendeleo ya watu wa Tanzania.

Shaka, amefafanua kwamba lengo kuu la CCM iliyozaliwa Februari 5, 1977 kutokana na ridhaa ya wanachama wa vyama viwili, ni kuongoza mapambano magumu ya kudumisha na kumarisha uhuru wa nchi na Watanzania wote.

Amesema kuwa katika kipindi cha miaka 45 ya uhai wake, CCM imefanya mengi mazuri kama ilivyokuwa kwa TANU na ASP, imeendelea kuwaongoza Watanzania sio tu katika kulinda uhuru wa nchi ya bali pia katika harakati za kujiletea maendeleo, mafanikio yanayoonekana katika utekelezaji wa sera zake.

Amesema mafanikio makubwa yaliyofikiwa kwa kipindi hicho ni kudumu na kuimarika kwa Muungano ambapo changamoto zake zimekuwa zikitatuliwa na hatimaye kuondosha manung’uniko miongoni na kuongeza upendo na mshikamano kwa Serikali zote mbili.

Shaka, amefafanua kwamba mafanikio hayo yamefikiwa kutokana na mfumo madhubuti na imara wa kisiasa uliojengeka ndani ya CCM.

Amesema ndani ya kipindi hicho cha miaka 45, Tanzania imepiga hatua kubwa kimaendeleo katika sekta ya miundombinu ya barabara, umeme,afya,elimu,teknolojia,kilimo na uvuvi.

“ CCM ina mengi ya kujivunia katika kipindi cha miaka 45 toka izaliwe, imefanya mengi makubwa katika kuimarisha Demokrasia,uchumi,maendeleo na misingi imara ya kiutawala.

Mafanikio hayo yanatokana na misingi imara ya kisiasa na kiuongozi iliyorithishwa na Vyama vya ASP na TANU vilivyoacha mazingira rafiki ya kimfumo yanayokifanya Chama kuwa imara siku zote.”, alisema Shaka.

Katika maelezo yake Shaka, amesema ndani ya kipindi hicho CCM imekuwa mwalimu wa Demokrasia,sikivu na kuheshimu uwepo wa vyama vingine vya kisiasa vilivyopo nchini.

Kupitia mkutano huo Katibu huyo wa NEC, aliyataja mafanikio mbalimbali yaliyopatikana kuwa ni pamoja na CCM kuwa na mtaji wa kiuchumi wa zaidi ya Shilingi Trioini 1.5.

Ameeleza kwamba kiwango hicho cha mtaji ni miongoni mwa vigezo mahsusi vinavyotyofautisha CCM na vyama vingine ya kisiasa nchini na barani Afrika kwani kina uwepo wa kujiendesha chenyewe kiuchumi na kimapato.

Mafanikio mengine amesema ni namna CCM kilivyokuwa na mfumo imara wa kuchagua na kuteua viongozi kwa kufuata kanuni,taratibu na Katiba ya Chama ya mwaka 1977.

Ameongeza kuwa mafanikio mengine makubwa ni kuimarika kwa Umoja na Mshikamano sambamba na amani na utulivu ambayo ni matunda yanayowanufaisha wananchi wote bila kujali tofauti zao za kisiasa.

“ Nchi inapokuwa na amani wananchi wa makundi yote wanapata fursa pana ya kufanya shughuli zao za kujiletea maendeleo, kwa sasa kila Mtanzania ana uhuru wa kusafiri na kuishi popote ndani ya nchi hii bila kusumbuliwa”, alisisitiza

Amesema CCM ina muundo imara wa kiungozi kuanzia ngazi za mashina hadi Taifa na maamuzi yote ufanyika kwa kufuata vikao halali, mafanikio hayo hayapo katika chama chochote cha kisiasa nchini.

Shaka, amesema CCM inampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wake Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi mzuri wa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2022.

Amesema kasi ya kiutendaji ya Rais Samia ni kielelezo tosha cha kuonyesha Dunia kuwa Tanzania ina kiongozi imara,mchapakazi,mzalendo,mbunifu,mtetezi wa haki za makundi yote  na kinara wa Diplomasia.

Katibu huyo wa NEC, amemtaja Rais huyo kuwa ni alama ya ushindi wa kudumu katika uwanja wa Demokrasia nchini unaotafsiriwa na CCM kuwa ni ushindi uliotukuka katika nyanja za kisiasa.

Akijibu hoja za baadhi ya waandishi wa habari, amefafanua kuwa lengo la kufanyika kwa kilele cha maadhimisho hayo Mkoani Mara ni kumuenzi Rais wa kwanza wa Tanzania hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere kutokana na mchango wake mkubwa wa kimaendeleo alioufanya enzi za uhai wake na kuiheshimisha Tanzania Kiaifa na Kikanda na Kimataifa.

Akizungumzia maadhimisho ya kilele cha sherehe hizo amesema CCM inawaalika Wananchi wote wa Mkoaa wa Mara, Mikoa jirani na Watanzania wote kuhudhuria sherehe hizo zitakazofanyika Februari 5, 2022 na zitaanza na matembezi ya mshikamano yatakayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.



 

 

 

   

KARIBUNI MKOANI MARA JAMBO LA LETU LINATIKI 05/02/2022.


MUONEKANO wa maandalizi ya sherehe ya Siku ya Kilele cha kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kitaifa ambapo sherehe hizo kwa mwaka huu zinafanyika Mkoani Mara Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan.

 





 



Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Mwamtum Dau Haji amekikabidhi jezi kwa timu mbili za wanawake 

Bungi na Kiembesamaki. zenye Thamani ya shilingi Laki mbili na elfu sabini.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Mwamtum Dau Haji amefungua michezo ya mechi za tombe la mbuzi zinaendela katika kiwanja cha
 

Bungi kwa kuanza kuchezwa na wanawake time ya Bungi City na Kiembe samaki na mwisho wa mchezo Bungi waliibuka kwaushindi wa maili moja na 

Mhe. Mwamtum Dau Haji aliwakabidhi timu zote mbili zawadi wa jezi kwa kila mmoja.




Pia mchezaji wa kiembe Samaki amesema kuwa wachezaji wenzake kunawengine wanajifunza wale wangle wanao weza wanatakiwa kuwasaidia 

Wanzao Katina kuwagawia pasi ilikuwawezesha kujifunza na amewataka wazazi wawaluhusu watoto wao wa kike kucheza mira wa miguu kwani 

Michezo his siuhuni na wanajiweka fiti kimwilina kiakili,  

MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA KUSINI UNGUJA MH. MWAMTUM DAU HAJI AMETEMBELEA KIKUNDI CHA CHAZA MALI


Bahati Issa akimwelezea jinsi kikundi icho kilivyoanza na kumuonesha usajili wa kikundi icho Mhe Mwamtam Dau Haji.


MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa kusini Unguja Mhe. Mwamtum Dau Haji akimkabidhi shilingi Laki mbili mmoja ya mwanakikundi kwa jili ya kuongeza mtaji kikundi icho cha Chaza Mali.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Mwamtum Dau Haji amewatembelea wanakikundi cha Chaza Mali kilichopo Kikungwa na kuwakabidhi shilingi Laki mbili kwa jili ya kukikuza kikudi icho. 

Na kuwataka wasivunjie moyo atakama kwasasa kinawanachama wachache kutoka na wanachama wengine kujito, ivyo inatakiwa kufanya

Kazi kwa midi na kuongeza ushilikiano ili kukuza kikundi icho na kitakapo kuwa kikubwa basi wale wanachama waliojitoa watalejea, 

kwa ivyo amewataka pia kulejea na biashara Yao ya zamani ya chaza na makome kwani inasamani sana kwa sasa tukiwa katika uchimi Wa bluu ilikumuunda mono Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi.


Piawa aliwaba msaada wa shilingi laki Mbili Kwa afili ya kuwaongezea mtaji wanakikundi hao na amewataka kuendelea kukimalisha kikundi icho

Ilikuoneza wanachama.



MMOJA kati wa mwanakikundi akimkabidhi kawa Mhe. Mtumtum Dau Haji kama zawadi.


Bahati Issa Suleiman mwanachama wa kikundi cha Chaza Mali nae pia amewaonda viongozi wengine kujitokeza kutoa msaada kwa wanakikundi

icho Kama alive jitokeza Mhe. Mwamtum Dau Haji. 


Pia ameitaka Serikali kuwasaidia wajasilia mali kwa kuwatafutia solo la bihashara na kuwapatia mikopo au vitendea kazi ilikuendele kukiimalisha kikundi chao na kujikwamua kiuchumi, kwani kukundi icho kilianza mwaka 2005 na kusajili wa mwaka 2009 na kikundi hicho kinajishilicha na kusuka mikoba, makawa, mikeka, uzaji wa vyungu na vyombo via plastiki.

MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA ASHA ABDALLAH JUMA AMETOA MSAADA WA VYAKULA KWA ALIOPATWA KWA AJALI YA KUUNGULIWA NA MOTO NYUMBA ZAO

WANAWAKE waliopata majanga ya kuunguliwa na moto katika nyumba zao zilizopo Mji Mkongwe wamemshukuru Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mjini Asha Abdallah Juma kwa msaada wa vyakula aliyowapatia kwa ajili ya kujikimu na familia zao.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo kutoka kwa Mbunge huyo Dorisi Rashid ambaye ni mmoja waliopata maafa hayo alisema  vyakula hivyo vitawasaidia kwa namna moja ama nyingine kutokana na kuwa mara nyingi majanga ya aina yoyote uwahadhiri zaidi wanawake kwani wao ndio walezi wa familia zao.

"Sisi wanawake ndio tunakuwaga waathirika sana kwani sisi ndio walezi wa familia hizi baba anaweza kukimbia zake lakini mwanamke huwezi ukiangalia watoto kulea ni jukumu letu kuhakikisha watoto wanakula na wanakwenda shule hivyo msaada huu utatusaidia sana sitopata tabu kufikiria kupata mchele,sukari,mafuta ama maharage,"alisema   



Dorisi alisema mpaka sasa ni miezi miwili tangia kutokea kwa ajali hiyo ya moto ambapo miongoni mwa familia nane zimeathirika na ajali hiyo na wamepewa makazi ya kujihifadhi katika nyumba za kuwahifadhia wazee eneo la Sebuleni hivyo bado wanahitaji msaada zaidi.

Naye Maimuna Hassan Ame alisema anashukuru kwa kupata msaada huo wa vyakula ikiwemo mchele,mafuta,unga,sukari na maharage na kwamba ameonyesha dhamira yake ya kiungwana kama mwanamke mwenzao katika kuwasaidia wanawake wenzao.

"Tunashukuru kwa kupata msaada huu wa vyakula kwani mpaka sasa ni muda mrefu takribani miezi miwili tangia ajali hii ya kuunguliwa na nyumba zao itokee tunawaomba wanawake wenzetu nao wajitokeze watusaidie kama vyakula na ikiwezekana hata fedha za kujikimu kwani watoto zetu wanakwenda shule wanahitaji nauli na mambo mengine,"alisema 

Akiwakabidhi msaada huo kwa niaba ya Mbunge huyo Mwenyekiti wa mkoa wa Mjini Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania ya Chama Cha Mapinduzi(UWT) Ghanima Sheha Mbwara alisema siku zote mwanamke ni mlezi katika familia hivyo mbunge huyo ameamua kutoa msaada huo ikiwa kama mzazi kwa familia hizo zilizopata maafa hayo.

"Ni kawaida UWT kujitoa katika kuwasaidia wanawake wenzao hasa katika wakati wanapopata maafa ya aina hii na maafa mengineo hivyo Mbunge huyu akiwa amechaguliwa na wanawake wenzao tena katika mkoa huu ameogusa kuwasaidia wanawake hawa,"alisema 

Alisema siku zote wanawake wanakuwa watu wa kuungana katika kusaidiana na kwamba hiyo ndio tabia yao hivyo kitendo cha Mbunge huyo wa vitimaalamu kuwasaidia ni dhahiri imeonyesha dhana hiyo ya wanawake kuungana.

UCHAGUZI WA NAFASI YA MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA KUPITIA BARAZA LA WAWAKILISHI

Kikao cha Wawakilishi wa Chama Cha Mapinduzi kupitia Baraza la Wawakilishi, Kimefanya uchaguzi wa kuwachagua Wawakili watatu kuwa Wajumbe wa Halmashauri  Kuu ya   CCM Taifa  (NEC).

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na pia Mkamu wa Rias wa Pili wa Zanzibar MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLA akitumbukiza karatasi ya kupigia kura katika sanduku la kura,



Katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa AFISI KUU YA CCM KISIWANDUI ZANZIBAR amnacho kimeongozwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLA, kimewachaguwa  NDG. JAMAL KASSIM ALI, ND. MASOUD ALI MOHAMMED NA  RIZIKI PEMBE JUMA Kuwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.


Pia amewataka Wajumbe Waliochanguliwa  kiwakilisha vyema kupitia misingi ya  CHAMA CHA MAPINDUZI kufuatia Katiba, Sheria, Kanuni, Miongozo na maelekezo ya CHAMA CHA MAPINDUZI. kufanya hivyo kutawajengea  uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa na kukiongezea sifa  CHAMA CHA MAPINDUZI kwa kusimamia demokrasia na uongozi bora.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Saadall (mabodi) akiwa katika kikao cha uchaguzi wa nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa katika Ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar. 



CCM ZANZIBAR MPYA