RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK HUSSEIN ALI MWINYI AMEAHIDI MASHIRIKIANO KWA UNICEF

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameliahidi Shirika la Umoja wa Mataifa linalowahudumia Watoto duniani (UNICEF) kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Nane itaendeleza mushirikiano na Shirika hilo ili kuhakikisha watoto wanapata haki zao za msingi.

Rais Dk. Hussein aliyasema hayo leo Ikulu Jijini Zanzibar wakati alikutana na  Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalowahudumia Watoto duniani (UNICEF) nchini Tanzania Bi Shalini Bahuguna ambapo mbali ya mazungumzo hayo Mwakilishi huyo alifika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha.

Katika maelezo yake Rais Dk. Hussein Mwinyi alitumia fursa hiyo kwa kulipongeza na kulishukuru Shirika la UNICEF kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuhakikisha malengo ya Shirika hilo yanafikiwa hapa Zanzibar ikiwa ni pamoja na kuimarisha ustawi wa watoto kwa kusaidia huduma mbali mbali zikiwemo zile za kijamii.

Rais Dk. Hussein alisema kwamba Serikali ya Awamu ya Nane iko tayari kushirikiana na Shirika hilo katika maeneo ya kipaumbele yaliyowekwa katika kuhakikisha mafanikio yanafikiwa.

Aidha, Rais Dk. Hussein alitumia fursa hiyo kulipongeza Shirika hilo kwa kuendelea kusaidia uimarishaji wa huduma za kijamii hapa Zanzibar hatua ambayo imekuwa ikiwasaidia watoto, vijana na hata wanawake.

Aliongeza kuwa mashirikiano yaliopo katika sekta ya afya kati ya Serikali na Shirika hilo ndio yameweza kuleta mafanikio ya kupunguza vifo vya kina mama na watoto hapa Zanzibar.

Pia, Rais Dk. Mwinyi alimuahidi Mwakilishi huyo wa UNICEF nchini kwamba changamoto zinazowakabili watoto likiwemo suala la ajira kwa watoto, ustawi wa watoto wa kiume katika sekta ya elimu vyote hivyo vinafanyiwa kazi.

Rais Dk. Hussein alieleza kuvutiwa na mikakati pamoja na programu mbali mbali zilizowekwa na Shirika hilo hapa nchini katika kuhakikisha linaendelea kuwasaidia watoto katika nyanja mbali mbali zikiwemo huduma za elimu, afya na uwezeshaji.

Sambamba na hayo, Mwakilishi huyo alipongeza juhudi za Serikali zilizofikiwa katika kupiga hatua za kupambana  na vifo vya akina mama na watoto na kuweza kupunguza idadi kubwa ya akina mama na watoto wanaofariki wakati wa kujifungua.

Alieleza kwamba miongoni mwa mikakati iliyowekwa na Shirika hilo ni kuhakikisha huduma za afya zinaongezeka ikiwa ni pamoja na kuongeza vifaa katika hospitali mbali mbali hapa Zanzibar sambamba na kuweka ustawi katika sekta ya elimu.

Alieleza azma ya Shirika hilo ya kuziendeleza programu ziliopo na kuziongeza zaidi kwa lengo la kupata mafanikio zaidi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha watoto wanapata haki zao za msingi zikiwemo huduma zote za kijamii.

Nae kwa upande wake Bi Maha Damaj ambaye ni Mkuu wa Ofisi za UNICEF Zanzibar alieleza juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Shirika hilo katika kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa  mashirikiano ya pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Nane katika kuhakikisha

No comments:

Post a Comment